May 25, 2018



Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa, amesema kikosi chao kipo tayari kukabiliana na Ruvu Shooting katika Uwanja wa Taifa leo.

Mkwasa amesema wachezaji wote wako tayari kwa mchezo wa leo huku akieleza kuwa mechi itakuwa ngumu kutokana na Ruvu Shooting kuonesha kiwango kizuri katika mechi kadhaa ilizocheza hivi karibuni.

Yanga inangia dimbani ikipigania nafasi ya pili ili kuweza kuwa makamu bingwa wa ligi. hivyo inahitaji kushinda mchezo wa leo na ujao dhidi ya Azam FC ili kufanikiwa maadhimio hayo.

"Wachezaji wetu wako tayari kkabiliana na Ruvu leo, tunajua mechi itakuwa ngumu kutokana na wenzetu kuonesha kiwango bora katika mechi zilizopita, tumejiandaa" amesema Mkwasa.

Aidha, Katibu huyo amewaomba wapenzi na mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi Uwanjani ili wakatoe hamasa kwa wachezaji.

Mkwasa amesema mapema baada ya mechi hiyo wataanza maandalizi ya kukabiliana na Azam FC, mchezo ambao utakuwa wa kuhitimisha safari yao katika ligi msimu huu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic