ENGLAND YAIFUNGASHIA VIRAGO PANAMA KOMBE LA DUNIA KWA KIPIGO CHA MBWA KOKO, KANE APIGA HATTRICK
England imeonesha ubabe wa kutosha katika mchezo wa kundi G dhidi ya Panama kwa kuipa kipio kikali cha mbwa koko cha mabao 6-1 kwenye michuano yaKombe la Dunia nchini Urusi.
Mabao matatu ya England yamewekwa kimiani na Harry Kane ambapo amefunga mawili kwa njia ya penati.
Mabao mengine ya England yamewekwa kimiani na John Stones aliyefunga mawili huku Jesse Lingard naye akitupia moja.
Panama imejipatia bao pekee la kufutia machozi kupitia kwa Nahodha wake, Felipe Baloy mnamo dakika ya 78.
Matokeo hayo yanaifanya Panama kuaga rasmi mashindano hayo na kuiacha England ikifikisha alama 6 mpaka nafasi ya kwanza ikiiacha Ubelgiji kwa utofauti wa mabao ya kufuna na kufungwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment