CRISTIANO RONALDO JR AJIUNGA NA JUVENTUS
Cristiano Ronaldo Junior, mtoto wa mwanasoka nyota duniani, Ronaldo, anayeichezea Juventus, amejiunga na kikosi cha watoto walio chini ya umri wa miaka tisa cha klabu kwa ajili ya mafunzo ya soka yanayojulikana kama Pulcini 2010.
Kwa mujibu wa Calciomercato ambaye ni ‘mshikaji’ wa Ronaldo, mtoto huyo alicheza na watoto wengine wa watu maarufu na alionyesha umahiri mkubwa.
Kituo hicho kilianzishwa, miongoni mwa malengo yake, kuendeleza vipaji vya watoto ambao baba zao nao walikuwa nyota wa soka.
Baba yake alijiunga na Juventus msimu huu baada ya kukaa kwa mafanikio makubwa na klabu yaReal Madrid.
0 COMMENTS:
Post a Comment