August 20, 2018


Kipa wa Liverpool Loris Karius, 25, anafanya mazungumzo na Besiktas, huku mkuu wa Reds Jurgen Klopp akiridhia kuondoka kwa Mjerumani huyo. (Mirror)

Manchester City inataka kuongeza mkataba wa mlinzi wa England John Stones wenye thamani ya £120,000 kwa wiki. Mkataba wa mchezaji huyo kwa sasa unaendelea hadi 2022. (Sun)

Kipa wa Uhispania David De Gea, mwenye umri wa miaka 27, anakaribia kusaini mkataba mpya wa thamani ya £200,000 kwa wiki na Manchester United. (Mirror)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Chelsea Ruben Loftus-Cheek, mwenye miaka 22, atazungumza na maafisa wa klabu wiki hii kuhusu mustakabali wake. Mchezaji huyo wa kimataifa ataomba kuhamishwa kwa mkopo iwapo meneja Maurizio Sarri hatoweza kumhakikishia muda atakaoichezea timu hiyo. (Sun)

Beki wa Scotland Andrew Robertson hana haraka ya kusaini mkataba mpya Liverpool; na huenda hakutokuwa na majadiliano msimu huu kuhusu mkataba mpya wa mchezaji huyo wa miaka 24.(Liverpool Echo)

Leon Bailey - anayelengwa na Manchester United, Liverpool na Chelsea - amesaini mkataba mpya huko Bayer Leverkusen. Mshambuliaji huyo mwenye miaka 21 raia wa Jamaica alihusishwa na uhamisho katika msimu wa joto. (Goal)

Mshambuliaji wa Chelsea na timu ya taifa ya Uhispania Alvaro Morata, 25, anasema "hapakuwa na fikra yoyote" kwamba angeondoka msimu huu, licha ya uvumi kuhusu mustakabali wake. (Mail)

Kutoka BBC

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic