Abdallah amesema sababu za kujiweka kando ni kuwaachia viongozi wengine waje na mawazo mampya ndani ya klabu ambayo inakuja na muundo mpya wa uongozi.
Kaimu huyo aliyekuwa anapewa nafasi kubwa zaidi ya kuchukua fomu, hakuweza kufika kwenye makao makuu ya klabu hiyo iliyo mitaa ya Msimbazi, Kariakoo kwa ajili ya kuchukua fomu hiyo.
Abdallah ameeleza kuwa wakati wa kuitumikia Simba umeshamalizika kama kiongozi lakini ataendelea kuwa mshauri kwa ajili ya kuiimarisha klabu kwa ujumla.
kiongozi huyo alichukua nafasi ya Evans Aveva ambaye alikuwa Rais wa klabu hiyo ambaye sasa ameshikiliwa na mahakama kutokana na makosa ya matumizi mabaya ya fedha.








0 COMMENTS:
Post a Comment