September 5, 2018


Akiwa na kikosi cha Mbao FC, Kocha Amri Said 'Stam', amefanikiwa kuipa rekodi ya aina yake timu yake mpya kwa kuiweka kileleni kwa msimamo wa ligi tangu ipande daraja.

Katika mechi tatu za ligi, Mbao imefanikiwa kuibuka na ushindi kwenye mechi mbili na kwenda sare moja hivyo kuifanya kuvuna alama 7.

Matokeo hayo yameipa Mbao FC rekodi ya aina yake kwa kuivunja ya aliyekuwa Kocha wa timu hiyo, Etienne Ndayiragije ambaye kwa sasa yupo KMC ya Dar es Salaam.

Unaambiwa katika msimu wa kwanza iliopanda daraja, Mbao ilicheza mechi nne na kuvuna alama moja pekee huku na uliofuatia ikipata alama nne katika michezo minne.

Rekodi hiyo inazipiku timu za Simba na Azam ambazo zimeshacheza mechi mbili na zikiwa na alama 6 kwa kila mmoja huku Yanga ikiwa na 3 ikicheza mechi moja.

Licha ya kuweka rekodi hiyo, Stam amesema bado wana safari ndefu ya kuhakikisha wanafanya vizuri kutokana na upinzani wa timu zilizopo.

Kocha huyo alisajiliwa na Mbao akitokea Lipuli FC mapema baada ya msimu wa 2017/18 kumalizika.


3 COMMENTS:

  1. Sasa rekodi gani ya Simba mbao aliyoipiku? Hovyoooo.

    ReplyDelete
  2. Hawa waandishi wanatoka wapi Mbona siwaelewi wajinga Sana mtu anajiandikia anavyoona pumbavu Sana mwandishi pimbi.

    ReplyDelete
  3. Blogu hii imekuwa mbovu na ya kizushi. Sababu ni ukanjanja wa waandishi na kukosa maadili.Zuberi blog iko mbele sana kwa kuandika habari za utafiti nä ukweli.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic