October 3, 2018


Manchester United walishindwa kumpunguzia shinikizo meneja wao Jose Mourinho baada ya kutoka sare tasa dhidi ya Valencia katika mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya iliyochezewa ugani Old Trafford.

United, ambao wanapitia mwanzo mbaya zaidi wa ligi katika kipindi cha miaka 29, walianza vyema kutokana na nguvu za Marcus Rashford na Alexis Sanchez waliorejeshwa kikosini.

Hata hivyo, wageni hao kutoka Uhispania waliimarika kadiri mechi ilivyosonga na wenyeji wakaanza kusambaratika.

Valencia ndio waliopata nafasi nzuri kabla ya mapumziko na baada ya mapumziko kabla ya United kuanza kuimarika tena.

Rashford alitikiza mwamba wa goli kwa frikiki, lakini Valencia walifanikiwa kulinda lango lao hadi mwisho wa msimu.

Sasa, United wamecheza mechi nne bila kupata ushindi.

United wamo nafasi ya pili katika Kundi H wakiwa na alama nne, mbili nyuma ya viongozi Juventus waliowalaza vijana wa Uswizi Young Boys 3-0 na ambao watakuwa wageni wa mashetani hao wekundu Old Trafford mnamo 23 Oktoba.


Mchezaji wa zamani wa United Cristiano Ronaldo anatarajiwa kucheza mechi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic