October 3, 2018




Klabu ya Yanga imeandika barua kwenda Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakieleza wanataka kuona TFF ichukue hatua kuhusiana na kitendo cha kiungo wa Simba, James Kotei.

Kotei alionekana akimpiga Gadiel Michael katika mechi ya watani Simba na Yanga, Jumapili iliyopita.

Msemaji wa Yanga, Dismas Ten amesema wameamua kufanya hivyo kama klabu wakionyesha wamekerwa wamekerwa na hali hiyo.

“Kama klabu hatuwezi kukaa kimya kwa vitendo ka hivyo vinatokea, tumeandika baraua.

“Sasa tutawaachia TFF wenyewe tuone kama wanachukua hatua au la, lakini sisi tumeonyesha namna tulivyokerwa na vitendo ambavyo si vya kiungwana,” alisema.

8 COMMENTS:

  1. WAPENI MAJIBU WANACHAMA NA WAPENZI WENU LINI MATENGENEZO YA UWANJA WA KAUNDA UTAISHA? WAPENI MAJIBU YA UANZAJI WA MIPANGO YA JEZI, UCHAGUZI, A LINI MANENO YANAKUWA VITENDO????MMEHAIDI SANA!!!!! SASA NI WAKATI WA VITENDO......KWENYE YAFUATAYO
    1. UWANJA WA KAUNDA
    2. KOCHA MSAIDIZI WA KUMSAIDIA ZAHERA.....WATU WAMEONA MAPUNGUFU NI DHAHIRI KUWA BENCHI LA UFUNDI LINAHITAJI KUIMARISHWA KAMA MNATAKA KUCHUKUA UBINGWA
    3. UCHAGUZI
    4. MABADILIKO YA MFUMO WA UENDESHWAJI
    5. USAJILI WA DIRISHA DOGO MMESHAANZA KUWATAFUTA WACHEZAJI WA KUONGEZWA NA KUWAPA MIKATABA YA AWALI?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hii copy na pachika kila habari...inaboa sana

      Delete
  2. Mmesahau watema mate...K.Yondani

    ReplyDelete
  3. Madhali mmekerwa bila ya shaka TFF itayafanyia kazi matakwa yenu kwasababu yanga ni taasisi kubwa sana sio yakupuuzwa

    ReplyDelete
  4. Hovyo kabisa Yanga. Kama kweli mmekerwa na kukureka jitoweni kwenye Ligi tutajua kweli mmekereka. Hamuwezi kuwafundisha kazi viongozi viburi kama wa TTF waliokuwa na kiburi cha kuwaacha wachezaji wa kuwapa ushindi uganda na kubaki kufurahia sare tasa.

    ReplyDelete
  5. Mbona hawajaandika barua ya kukerwa na kichwa alichopigwa Mohd Hussein na Dante?TFF ilichukua hatua gani kwa Kelvin Yondani alipomtemea makohozi Asante Kwasi? TFF tupeni majibu.

    ReplyDelete
  6. Hata mmimi siungi mkono vitendo vya kiungwana michezoni lakini tukumbuke ikiwa kwa kungwi kunaliwa na kwa somo pia kuliwe.........yumkini kama mnakerwa na vitendo ambavyo si vya kiungwana mngenza kuonesha mfano sio zilongwambali zitendwa mbali................Ngoma alimpiga Kessy akiwa Simba Mlikereka? Yondani alimtemea mate Kwasi, Mlikereka? UUNGWANA HUANZIA NYUMBANI

    ReplyDelete
  7. Kadhalika nawasihi muangalie kwa makini tukio la Mchezaji Vicen Chikupe akimtwanga Kichwa Mohamed Hussein

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic