November 20, 2018


Upana wa kikosi cha Simba kwa sasa umefanya baadhi ya wachezaji kukosa namba kikosi cha kwanza, Kocha Mkuu Patrick Aussems anataka kuwatoa wachezaji wanne kwa mkopo.

Habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa kwa sasa mpango wa kusajili dirisha dogo ni kwa nafasi mbili tu ambazo zimeelekezwa na kocha ila ametoa maagizo pia ya kutoa wachezaji wanne kwa mkopo.


"Kocha anataka kuwatoa wachezaji wanne kwa mkopo ili waweze kupata nafasi katika timu watakazokwenda kutokana na ugumu wa kupata namba jinsi ulivyo ndani ya kikosi chetu kwa sasa.


"Suala la wachezaji gani hilo bado hajaliweka mezani anatarajiwa kutoa ripoti ya majina ya wachezaji hao ambao watatolewa kwa mkopo hivi karibuni," kilieleza chanzo.


Tayari kuna timu ambazo zimetuma barua kuwaomba wachezaji kwa mkopo kutoka Simba ikiwa ni pamoja na African Lyon, Singida United na wachezaji wanaowaniwa sana ni Marcel Kaheza, Rashid Juma, Nicholus Gyan na Mohamed Rashid.

1 COMMENTS:

  1. "hawa hapa kuondoka simba", halafu ndani ya habari hatuwaoni. Mnatuzingua bhana.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic