November 28, 2018


Kikosi cha Simba kimefanikiwa kuanza vizuri leo katika mchezo wa Fainali za Mabingwa ya Afrika uliochezwa Uwanja wa Taifa kwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Mbabane Swallows FC ya Swaziland.

Mabao ya Simba yalifungwa na John Bocco dakika ya 7 akimalizia pasi ya Nicolus Gyan kisha akafunga bao la pili dakika ya 32 kwa mkwaju wa penati baada ya Emmanuel Okwi kuchezewa rafu na mlinda mlango wa Mbabane.

Mbabane waliweza kutikisa nyavu za Simba dakika ya 24 lililofungwa na Guevane Nzambe na kufanya kipindi cha pili kumalizika kwa bao 2-1.

Simba walirejea kwa kasi kipindi cha pili na kufanikiwa kufanya mashambulizi na wakafunga bao la 3 lililofungwa na Meddie Kagere dakika ya 83 baada ya mlinda mlango wa Mbabane kuteleza akiwa na mpira kisha dakika ya 90 Clatous Chama alifunga bao la 4 akimalizia pasi ya Hassan Dilunga.

Simba watatakiwa wasiruhusu bao wakienda ugenini ili waweze kusonga mbele katika hatua ya michuano hii kwa kuwa Mbabane sio timu ya kubeza

4 COMMENTS:

  1. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Eti wamatakata!ikiwa Simba mnatumia lugha rahisi sana.Ingekuwa Yanga imefunga 4 mngetumia maneno kama Mauaji au imefanya Maajabu!

      Delete
  2. Wenzenu kule binzubery wameandika Simba imetoa onyo Afrika..Nina hakika saleh jembe wangetumia maneno kama hayo ingekuwa timu yao wanayoifagilia imeshinda

    ReplyDelete
  3. Eti simba inatakiwa isiruhusu bao kama wanataka kusonga mbele!ovyo sana mwandishi tatizo uyanga unakusumbua ila utapata taabu sana.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic