Baada ya beki wa kulia wa Simba, Shomari Kapombe, kufanyiwa upasuaji wa mguu kufuatia kuumia enka kwenye kambi yaTaifa Stars nchini Afrika Kusini wachezaji na mashabiki wa Yanga wamemuombea dua apone haraka.
Kapombe alilazimika kubakia nchini humo kwa ajili ya kupatiwa matibabu, na tayari alifanyiwa upasuaji wa mguu wake katika hospitali moja kubwa kwenye Jiji la Pretoria, Afrika Kusini.
Mrisho Ngassa kiungo mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa ana imani beki huyo atarejea katika hali yake na Mungu atamsaidia apone.
Juma Abdul nahodha msaidizi wa Yanga naye pia alisema kuwa ni mapito ambayo wachezaji wanapitia hivyo Mungu atamsaidia atakuwa salama.
0 COMMENTS:
Post a Comment