Ofisa habari wa KMC, Anwari Binde amesema ugumu huo unatokana na ukweli kwamba kocha Mkuu wa KMC, Ettiene Ndayiragije alikuwa kocha wa Mbao awali hivyo mbinu zake zipo wazi kwa wapinzani wao.
"Ushindani utakuwa mkubwa ukizingatia kwamba mbinu zetu zipo mikononi mwa Mbao, tumejipanga kupata matokeo na muda utazungumza uwanjani kocha ametoa mafunzo makini yatakayosaidia wachezaji kutafuta matokeo," alisema.
KMC wamekuwa na matokeo mazuri hivi karibuni baada ya kupanda daraja kwa kuwa ipo ndani ya 10 bora kwenye msimamo ikiwa inashika nafasi ya 9 ikiwaacha mbali Tanzania Prisons ambao msimu uliopita walimaliza wakiwa nafasi ya nne.
0 COMMENTS:
Post a Comment