Kesi ya aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na wenzake, Selack Mesaki ambaye alikuwa Mhasibu
wa TFF, imesikilizwa leo ambapo shahidi wa 9 alitoa ushahidi wake katika
Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu, Dar, na kupokewa na Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri.
Malinzi anatuhumiwa
na makosa 28, huku 23 kati ya hayo yakiwa ni kufoji risiti za kuwa anaidai TFF
na kujipatia pesa zaidi ya dola laki 2 ambazo zinaonyesha zilianza kufojiwa
tangu Novemba 2013 hadi Julai 2016.
Shahidi wa tisa, alifikisha vitabu vya
risiti vilivyotumiwa na Malinzi kwa
ajili ya kutolewa fedha za mkopo kutoka kwake kwenda TFF, ambapo Wakili
Mashauri alikubali ushahidi huo baada ya shahidi kuzitambua.
Miongoni mwa risiti hizo ni zenye namba
00831 ya Mei 9, 2016 ambayo inaonyesha kuwa kiasi cha dola 8000, namba 00832 ya
Mei 9, 2016 inaonyesha alitoa dola laki
saba, risiti namba, 00870 ya Mei 27, 2016 ambayo ilitoa kiasi cha shilingi
milioni tano kwa ajili ya maandalizi ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17.
Risiti nyingine ni ile inayosomeka
namba 00931 ya Juni 16, 2016 ambayo aliikopesha TFF dola 10,000, risiti namba 00947 ya Agosti 2, 2016 iliyoonyesha
kuwa Malinzi alitoa dola 1,000 kwa ajili ya kuwezesha safari ya Afrika Kusini
ya Ayubu Nyenzi na Pelegrinius Rutayuga.
Aidha, ushahidi mwingine wa risiti
uliotolewa ni namba 010137 ya Septemba 21, 2016 ambayo inaonyesha Malinzi ameikopesha
TFF shilingi milioni 7, risiti namba 01042 ya Septemba 21, 2016 iliyotolewa
shilingi milioni tatu ikitoka kwa Malinzi kwenda TFF ikiwa ni posho kwa ajili
ya timu ya vijana chini ya miaka 17.
Pia kuna risiti namba 01071 ya Septemba
22, 2019 ambayo inaonyesha imetolewa dola elfu 15 kutoka kwa Malinzi ikiwa ni
mkopo kwa ajili ya safari ya timu ya vijana chini ya miaka 17 kwa ajili ya kwenda
Rwanda na Congo.
Baada ya kuwasilisha ushahidi huo,
mawakili upande wa washtakiwa wakiongozwa na Richard Rweyongeza, walimuhoji shahidi
huyo mambo mbalimbali kuhusiana na ushahidi huo, huku pia wakiomba siku
nyingine mashahidi waweze kusikilizwa watatu na siyo mmoja ili kesi iende
haraka.
Baada ya pande zote mbili kusikilizwa,
Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 18, mwaka huu.
Mbali nan Malizi, washtakiwa wengine ni aliyekuwa Katibu wa TFF, Nsiande Isawayo Mwanga, Meneja wa Ofisi ya TFF, Miriam Zayumba na karani, Flora Rauya.
0 COMMENTS:
Post a Comment