MBADALA WA KAPOMBE SIMBA AANZA NA YANGA KWA NAMNA HII
Baada ya kutua nchini, beki mpya wa Simba, Muivory Coast, Zana Oumar Coulibaly amesema hawafahamu watani wao Yanga huku akiingia hofu ya ubora wa wachezaji wanaounda kikosi hicho.
Beki huyo alitua nchini juzi Jumatano saa 11 jioni akitokea nyumbani kwao Ivory Coast ambaye alitua nchini kwa ajili ya kusajiliwa katika usajili huu wa dirisha dogo linalotarajiwa kufungwa Desemba 15, mwaka huu.
Simba inataka kumsajili beki huyo kwa ajili ya kuziba nafasi ya Shomary Kapombe ambaye alivunjika kifundo cha mguu na kufanyiwa operesheni nchini Afrika Kusini.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Coulibaly alisema anaiheshimu Yanga kutokana na ukubwa wa klabu hiyo huku akiamini siku atakayokutana nayo mchezo utakuwa na upinzani mkubwa.
Coulibaly alisema, upinzani utatokana na ubora wa Yanga ambao anaamini ina wachezaji wengi wenye uwezo mkubwa, hivyo anausubiria mchezo huo wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.
“Mimi siifahamu Yanga, lakini kuanzia hivi sasa nitaanza kuifuatilia kwa ukaribu baada ya kupata taarifa kuwa ndiyo wapinzani wakubwa wa Simba, hivyo ni lazima niwajue.
“Ninaamini Yanga ni timu bora yenye wachezaji wazuri na kazi kubwa itakuwepo mara nitakapokutana nao, mchezo utakuwa na ushindani mkubwa kutokana na upinzani utakaokuwepo.
“Nimepanga kuanza kuifuatilia hivi sasa Yanga baada ya kujiunga na Simba na nitaiangalia kwa kupitia mechi za hivi karibuni ambazo imezicheza,” alisema Coulibaly.
Mchezaji asajiliwe simba alaf aanze kuifuatilia yanga kwa kipi walichonacho hao vyura kaja kucheza so kufatilia hao ngada fc mwandishi kaandika uharo kabisa khaaaa!
ReplyDeleteNa jamaa hastahili kabisa kuwafikiria hao Yanga kulingana na nafasi yake anayochezea, kwani hajaambiwa kuwa yanga wenyewe kwa sasa wakikutana na Simba wao kazi yao ni kupaki basi, labda afikirie jinsi ya kupeleka makrosi kwa washambuliaji, lakini huku kwenye nafasi yake ya beki, aondoe hofu kabisa.
ReplyDelete