Baada ya kupoteza pointi tatu nyumbani mbele ya Yanga, kocha msaidizi wa timu ya Prisons, Ismail Seleman amesema kuwa makosa ya mabeki yameigharimu timu.
Prisons wana pointi 10 wamepoteza michezo 7 kati ya 15 waliyocheza wakiwa na sare 6 na wameshinda mchezo 1 pekee.
"Tulianza vizuri na hakukuwa na tatizo kubwa ambalo limetugharimu zaidi ya mabeki kukosa utulivu wakati wa mchezo hali iliyosababisha tuweze kufungwa bao 3-1.
"Tatizo la washambuliaji tumeliona nalo tutalitendea kazi kwa kuwa taratibu wanaanza kuelewa kile ambacho wanatakiwa kufanya hivyo baada ya muda watarejea kwenye ubora," alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment