January 13, 2019



KOCHA Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema anafurahishwa na sapoti ya mashabiki anayopata akiwa ndani ya Yanga hali inayomfanya afanye kazi kwa juhudi.

Zahera amekuwa kipenzi cha mashabiki pamoja na wachezaji kutokana na namna anavyoibuka kifua mbele kwa kupindua matokeo kila anapozidiwa mbinu.

Zahera amesema mashabiki wa Tanzania ni tofauti na wa nchi ya Congo kwani kule kila ukanda una timu yake tofauti na ilivyo Tanzania.

"Mashabiki wanapenda mpira na wanapenda timu zao, wanazipa sapoti kwa hali na mali hali ambayo inanifanya niwe na furaha kuwa ndani ya Yanga na ardhi ya Tanzania," alisema Zahera.

Matokeo ambayo alifanikiwa kupindua ni pamoja na mchezo kati ya Ndanda ambao alikuwa nyuma kwa bao moja na ule dhidi ya Tanzania Prisons ambao nao alikuwa nyuma kwa bao moja.

3 COMMENTS:

  1. Mashabiki wa Yanga mnaidhalilisha nchi kushangilia wageni ni mara mia bora mkaae nyumbani kuliko kuja uwanjani na kushangilia mwishoni aibu inawakuta Simba itashinda tu....huu ni mkakati (TFF, Simba wanachama, wageni, Serikali kuu, serikali ya mkoa na Jeshi la Polisi na wadhamini au wawekezaji wa klabu ya Simba) pointi 9....kwa mchina lazima....nguvu moja....ni kauli mbiu kwa vitendo....

    ReplyDelete
  2. Simba inaweza bhana! hilo lazima tulikubali. Hata wale jamaa zetu wa upande wa pili jana walikuja Taifa wakiwa na mabango yameandikwa "NO YOU CANT, SAOURA IS KISIKI CHA MPINGO", wale jamaa hata sikuwaona tena na bango lao! sijui walitokea mlango gani! nadhani hata kujuta walijuta juu ya muda na gharama walizotumia kuliandika bango lile!. Itawabidi mpende tu sasa, soka safi mmeliona tena la burudani, na bado magoli mmeyaona yote ni magoli ya akili na ya mateso makubwa kwa wapinzani. kubalini tu jamani.

    ReplyDelete
  3. Mbona comment zenu ziko nje ya mada husika?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic