IKIWA leo Arsenal ya kocha Unai Emery's itakuwa Uwanja wa Etihad kumenyana na Manchester City ya Pep Guadiola, kocha wa Arsenal amesema Guadiola ni mwalimu wake kwani anajifunza vitu vingi kupitia kwake.
"Huwa najifunza mengi nikiangalia timu za Guadiola kuanzia Barcelona, Bayern Munich na City zote zilikuwa na wachezaji wazuri ila sifa kubwa ya Guadiola ni kuinoa kiwango chao. Kwa kweli yupo juu ya makocha wengine ulimwenguni.
Kocha wa ManCity, Guardiola ameonya kuwa baada ya timu yake kufungwa na Newcastel watakuwa tofauti dhidi ya Arsenal.
"Tumechambua kwa kina makosa tuliyofanya kwenye mechi yetu iliyopita na Newcastel, kwa kila hatua hatutarudia makosa hayo kwenye mechi yetu dhidi ya Arsenal," alisema Guardiola.
0 COMMENTS:
Post a Comment