February 27, 2019


KOCHA Mkuu wa Yanga Mkongoman, Mwinyi Zahera ametamka kuwa huyu wa sasa ndiye kiungo wake halisi, Pappy Tshishimbi anayemjua na si yule aliemkuta klabuni hapo.

Kiungo huyo hivi karibuni amerejea kikosini akitokea kwenye majeraha ya goti am­bapo awali alikosa nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza kutokana na kutoridhishwa na kiwango chake.

Tshishimbi alianza kurejesha kiwango chake na kupata nafasi ya kucheza kwenye mchezo wa ligi dhidi ya JKT Tanzania kabla ya baadaye kudhihirisha ubora wake dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kufanikiwa kum­dhibiti kiungo Mzambia, Claytous Chama.

Zahera alisema hakuwa­hi kuwa na ugomvi na Tshishimbi huku akitaja kushuka kwa kiwango chake ndiyo kulisaba­bisha apoteze nafasi ya kucheza katika kikosi chake cha kwanza.

“Tshishimbi niliwahi kumsema mbele ya waandishi ya habari kuwa anacheza bila kufuata maelekezo yangu kutokana na nafasi yake anay­oicheza namba sita, hatakiwi kupiga chenga na kukaa na mpira muda mrefu.

“Lakini yeye alikuwa akipiga chenga kitu ambacho nilikuwa sikitaki, yeye kazi yake ni kunyang’anya mipira na kupiga pasi kwa washambuliaji pekee ndani ya wakati ili kuhak­ikisha timu inapata ushindi.

“Kama unamfuatilia vizuri Kante (N’golo) yule kiungo wa Chelsea anavyocheza utakuwa umenielewa ni mchezaji am­baye haumuoni akikaa na mpira kabisa, kwenye michezo ya hivi karibuni nimeona ubora wa Tshishimbi anaweza kuisumbua timu yoyote kwa sasa,”alisema Zahera.

4 COMMENTS:

  1. Lakini ilibidi aweke wazi kuwa kashindwa kuipenya ngome ya akina wawa tu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ngome isiyopenyeka bongo. Nje ni uchochoro tu.

      Delete
  2. Pale mechi na SSC alikutana na muziki munene, so isingelikua kazi nyepesi kwake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mziki mnene bongo. Ukitoka nje unakuwa mziki nyanya

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic