March 18, 2019


Mahakama Kuu imezuia mali za mfanyabiashara maarufu nchini na Mwanachama wa Yanga, Yusuph Manji kutokana na madeni anayodaiwa na Benki ya NBC

Manji anadaiwa zaidi ya shilingi bilioni 25 ambazo ameshindwa kuzirejesha kwa wakati kwa mujibu wa mkataba hivyo kusababisha mali zake zilizopo Mwanza na Dar es Salaam ambazo ziliwekwa dhamana, kuzuiwa

Mali hizo zimezuiwa kwa oda mbili tofauti za Mahakama hiyo, zinazomzuia Manji kufanya muamala wa aina yoyote kuzihusu ikiwamo kuhamisha umiliki kama zawadi, kuuza au kuweka dhamana

NBC ilifingua kesi mwaka 2016 ikizishtaki kampuni za Farm Equip (T) Limited, Tanperch Limited na Quality Group Limited zinazomilikiwa na Kaniz Manji na Yusuf Manji kwa kushindwa kurejesha mkopo wa Sh15.9 bilioni.

4 COMMENTS:

  1. kila linapokuja suala la kufamyika uchaguzi Yanga yanaibuka matatizo mapya ya Manji
    nadhani hili linabidi lichunguzwe kwa undani Zaidi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwani wewe binafsi unashindwa nini kuchungunza kwa undani zaidi? uchaguzi na madeni anayodaiwa Manji inawahusu vipi Yanga?

      Delete
  2. Juu ya yote haya yanga bado wamo kumuandama kwakutaka hela

    ReplyDelete
  3. Yaani wasidai madeni yao kwa sababu Yanga wanataka kufanya uchaguzi!!!
    Fikra mufilisi dawa ya deni kulipa sio kutafuta mchawi.
    Ujinga ni maradhi.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic