March 1, 2019


KIKOSI cha Simba, Jumapili hii kinashuka uwanjani kupambana na Stand United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Simba itashuka katika mchezo huo, huku ikiwa na kumbukumbu ya kuibu­ka na ushindi wa nguvu hivi karibuni ilipopambana na Lipuli FC huko mkoani Iringa ambako ilishinda mabao 3-1.

Hata hivyo, uongozi wa benchi la ufundi la Stand United, umeweka wazi mipango yake iliyojiwekea kwa ajili ya kuhakikisha timu hiyo inaibuka na ushindi katika mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ush­indani mkubwa ambapo mbinu hizo zinahusiana na timu ya Yanga ambayo ni mahasimu wakubwa wa Simba.

Kocha Msaidizi wa Stand United, Athuman Bilali ameliambia Championi Ijumaa kuwa, wamejipan­ga vilivyo kwa ajili ya mechi hiyo na mbinu watakazotu­mia kupata ushindi katika mechi hiyo hazitakuwa na tofauti sana na zile wali­zozitumia dhidi ya Yanga na wakafanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0.

“Tunaiheshimu sana Simba, lakini katika mechi yetu ya Jumapili tutahakiki­sha tunaibuka na ushindi kutokana na mikakati yetu tuliyojiwekea.

“Mbinu ambazo tulizitu­mia tulipocheza na Yanga, ndiyo hizo tutakazotumia dhidi ya Simba ambayo ina washambuliaji wengi wazuri ambao tayari tume­shapata mbinu za kutosha kuwazuia kuhakikisha hawaipenyi ngome yetu,” alisema Bilali.

Simba kwa sasa ipo nafasi ya tatu katika msi­mamo wa ligi kuu ikiwa na pointi, 48 wakati Stand United yenyewe ipo nafasi ya 10 ikiwa na pointi 33. Yanga ndiyo inayoongoza msimamo huo ikiwa na pointi 61.

7 COMMENTS:

  1. We sema tu mwisho wa siku utalia sana

    ReplyDelete
  2. Kabla ya kuropoka ilibidi kujifunza kwa walokuwa na kele nyingi na baada ya kichapo kuangukakia pua na kutoweka

    ReplyDelete
  3. Yanga kabla ta kuwapa mchongo wenhine, kwanza ijipe mchongo wenyewe au kujipatia point 62 ndio wanaona mambo yamekwisha HAHAAA

    ReplyDelete
  4. Stand ndo wa kumfunda yanga, sio yanga kumfunda stand kwa sababu mfundaji alidundwa na mfundwa.

    ReplyDelete
  5. Yaan wanapata mbinu kwa m2 tlie mfnga sisi

    ReplyDelete
  6. Never fear an army of lions led by a sheep. but fear an army of sheep led by a Lion

    ReplyDelete
  7. Sasa wenyewe walipigwa moja bila,wakapigiwa mpira mwingi sana ,watasaidianaje na walio wapiga

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic