HAJI MWINYI KUMALIZANA NA AZAM
Imeelezwa kuwa beki wa kushoto wa klabu ya Yanga, Haji Mwinyi yupo kwenye mipango ya kusajiliwa na matajiri wa jiji la Dar es Salaam, Azam FC.
Taarifa zinasema Azam tayari walishaanza mazungumzo na mchezaji huyo ikiwezekana waweza kuwawahi Yanga ambao pia wana mazungumzo ya kuongeza naye mkataba mwingine.
Mwinyi ambaye amekuwa moja ya wachezaji tegemo ndani ya Yanga tayari mkataba wake unaelekea ukingoni ambapo baada ya msimu huu utakuwa umemalizika.
Kama akiondoka Yanga, Mwinyi atakuwa ameondoka kama mchezaji huru tayari kuwatumikia matajiri hao wa jiji la Dar
Nenda mwanangu ukapate kipato cha hakika
ReplyDelete