HIACE YAUA 7, YAJERUHI 12 KIGOMA
WATU saba wamefariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupasuka tairi la nyuma na kupinduka mkoani Kigoma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Ottieno, amesema ajali hiyo ilitokea jana saa 12 :15 jioni katika kijiji cha Mlela wilayani Uvinza.
Alisema gari hilo lililokuwa linatokea wilayani Uvinza kwenda Kigoma na majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Mkoa ya Maweni.
0 COMMENTS:
Post a Comment