May 7, 2019


STRAIKA namba moja wa Gor Mahia ya Kenya, Jacques Tuyisenge analipwa Sh.Mil 5.7 ndani ya Gor Mahia lakini anataka Yanga imlipe Sh.mil 18 mshahara asaini.

Meneja wa Tuyisenge ambaye pia ni Meneja wa Meddie Kagere, Patrick Gakumba ameliambia Spoti Xtra kuwa amewaambia viongozi wa Yanga mchezaji huyo anauzwa Sh 460 milioni.

“Katika mazungumzo ya hivi karibuni niliwaambia kuwa mbali na dau la usajili, nimewaambia wamuandalie mshahara wa dola 8,000 (zaidi ya Sh milioni 18) kwa mwezi.

“Fedha hizo zinaoneka kuwa ni nyingi lakini ni kidogo sana kutokana na kazi yake kubwa ambayo amekuwa akiifanya uwanjani.

"Jambo ambalo limesababisha timu mbambali za Afrika kuanza kuisaka vilivyo saini yake,” alisema Gakumba ambaye ni raia wa Rwanda.

CHANZO: SPOTI XTRA

3 COMMENTS:

  1. Jee mutamueeza, Simba ilitamka mwanzo kumtaka, lakini wakajiweka upande na kuwaachia yanga kuepukana na chokochoko

    ReplyDelete
  2. Hizo ni gharama kubwa sana lazima waangalie hali ya klabu kiuchumi

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic