May 2, 2019



HERITIER Makambo, mshambuliaji wa Yanga ameongeza kasi yake kwenye ufungaji wa mabao na kuifanya vita ya ufungaji bora kuzidi kunoga.


Bao lake alilopachika leo dhidi ya Prisons limemfanya awafikie wababe wa kutupia nyavu kwenye Ligi Kuu Bara, Meddie Kagere wa Simba na Salum Aiyee wa Mwadui ambao walianza kabla yake kutupia mabao 16. 

Anayefutia kwa kutupia bongo ni nahodha wa Simba, John Bocco akitupia 14 huku Eliud Ambokile wa Mbeya City, Said Dilunga wa Ruvu Shooting, Donald Ngoma wa Azam FC wakiwa wametupia mabao 10.
Mfungaji bora wa msimu uliopita alikuwa ni Emmanuel Okwi wa Simba ambaye alitupia mabao 20 na saa ana mabao 10 kwenye ligi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic