JACOB
Massawe aliyekuwa nahodha wa Stand United amejiunga na Gwambina FC.
Massawe
amejiunga na kikosi hicho kwa kandarasi ya mwaka mmoja kuitumikia timu hiyo
ambayo inashiriki Ligi Daraja la kwanza baada ya timu yake ya Stand United kushuka daraja.
Wachezaji
wengine ambao wamesajiliwa na Gwambina FC ni pamoja na Antonio Matogolo aliyekuwa
Geita Gold, Raizin Hafidhi aliyekuwa Coastal Union, Ibrahim Isihaka kutoka
Alliance, Malika Ndeule na Ibrahim Job ambao walicheza Ndanda FC.
Pia
aliyekuwa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Kelvin Sabato amejiunga na timu hiyo
kwa kandarasi ya miaka miwili.
Turudi kwenye "vumbi letu na usajili wa magazeti na mihemko ya ushabiki wa timu za Kariakoo zinazodumaza soka letu"
ReplyDelete