August 17, 2019



HARUNA Shamte, beki mpya wa Simba, mtaalamu wa mipira iliyokufa ambapo msimu uliopita alifunga jumla ya mabao 5 akiwa Lipuli na sasa amesaini kandarasi ya miaka miwili ndani ya Simba amesema ana imani leo wanabeba ngao ya jamii mbele ya Azam FC.

Azam FC  na Simba leo zitakuwa kazini kufungua pazia la Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza Agosti 23 kwa mchezo wa ngao ya jamii uwanja wa Taifa majira ya saa 1:00 usiku.

Akizungumza na Saleh Jembe, Shamte amesema kuwa wanatambua wapinzani wao Azam FC ni bora ila bado ubora wa kikosi cha Simba unawapa ushindi.

“Hakuna ambaye hatambui ubora wa kikosi cha Azam FC ndani ya timu ya Simba kwa sasa ila linapokuja suala la kikosi kipana kipo ndani ya Simba na hayo yataonekana uwanjani.

“Kila sekta kwa sasa imekamilika ni kikosi cha moto, mbinu za Kocha pamoja na ushirikiano uliopo ndani ya kikosi tuna imani ya kubeba ngao mbele ya wapinzani wetu,” amesema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic