August 17, 2019



NYOTA wa timu ya Simba, Meddie Kagere na Hassan Dilunga wamepania kuirejesha kwa mara ya pili ngao ya jamii makao makuu ya Msimbazi pale Kariakao mchezo utakaochezwa leo uwanja wa Taifa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Dilunga amesema kuwa maandalizi yamekamilika kinachosubiriwa ni wakati ili kutimiza malengo waliyojiwekea.

“Tuna kazi ngumu na tunajua haitakuwa kazi nyepesi ila uhitaji wa kushinda ni mkubwa ukizingatia kwamba msimu uliopita tulitwaa taji hili lazima tupambane kubaki nalo tena,” amesema.

Kwa upande wa Kagere amesema kuwa wana imani ya kupata matokeo mbele ya kikosi cha Azam FC hivyo mashabiki wawape sapoti kwani kazi itakuwa ngumu. 

Kagere na Dilunga msimu uliopita walitupia mabao 2 yaliyoipa taji la ngao ya Jamii Simba mbele ya Mtibwa Sugar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic