August 31, 2019



BRUNO Tarimo, maarufu kama Vifua Viwili, leo atakuwa na kazi moja ulingoni kupeperusha Bendera ya Tanzania kwenye pambano la raundi 12 dhidi ya  Mserbia, Scheka Gurdijeljac.

Pambano hilo la ubingwa wa Dunia linatazamiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na rekodi za Vifua viwili kutopoteza pambano zaidi ya kupoteza  moja kwa pointi kati ya mapambano 26 aliyocheza.

Pambano hilo linatarajiwa kuchezwa leo Agosti 31 nchini Serbia ukumbi wa Hala Pendik Novi Pazar.



Akizungumza na Championi Jumamosi Vifua Viwili  alisema kuwa :“Natambua kuwa watanzania wananiombea nitapambana kubeba ubingwa ili kupeperusha vema Bendera ya Taifa kikubwa sapoti kwani maandalizi yapo vizuri,” alisema Vifua Viwili.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic