August 31, 2019



KOCHA msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania,‘Taifa Stars’ Seleman Matola amesema kuwa ana imani kikosi kitakwenda kufanya kweli kwenye mchezo wao wa kufuzu Kombe la dunia dhidi ya Burundi.

Stars, itamenyana na Burundi Septemba 4 Uwanja wa Prince Louis Rwagasore, nchini Burundi kabla ya kurudiana nao uwanja wa Taifa, Septemba 8 mwaka huu.

Matola amesema kuwa wachezaji wana morali kubwa ya kupambana na kila mmoja anatimiza jukumu lake kwa wakati.

“Tuna kazi ngumu ya kufanya hasa ukizingatia tutakuwa ugenini jambo ambalo limetufanya tutumie muda mwingi kuwaandaa wachezaji wetu.

“Matumaini ya kufanya vizuri ni makubwa, kikubwa ni sapoti ya mashabiki kuelekea kwenye mchezo wetu kwani hesabu zetu ni kupata matokeo mazuri,” amesema.

2 COMMENTS:

  1. Kilalakheri Taifa Stars, Tunawaombea Muweze Kushinda Mechi Hiyo

    ReplyDelete
  2. Muzamiru Yasini yupo vizuri zaidi hivi sasa itapendeza kama jitihada zake zikaongezewa ndimu kwa kuitwa Taifa stars .

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic