September 1, 2019


KIKOSI cha Azam FC, leo kimeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Transit Camp kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Uhuru.

Azam FC ilianza kupachika bao la kwanza kupitia kwa Daniel Amoah kisha Donald Ngoma alipachika jumla ya mabao mawili na lile la kufutia machozi kwa Transit Camp likipachikwa kimiani na Samson Mkwangwa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Rajabu Bwamkuu, Kocha Mkuu wa Transti Camp amesema kuwa amejifunza kutokana na makosa kwenye mchezo huo.

"Tumepoteza kwa makosa yetu ni wakati wetu kujipanga upya kwa ajili ya wakati ujao, bado ninaijenga timu na wachezaji wanajua kazi yao kushindwa sio mwisho wetu tutaendelea kupambana," amesema. 

Trasnit Camp inashiriki Ligi Daraja la Kwanza ambayo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 14 na imepangwa kundi B.

1 COMMENTS:

  1. Moto huu ambao Azam wanao, Inabidi wauwashe hadi ligi kuu waweze kumng'oa Simba Ubingwa hapo ndo tutatambua kuwa Azam ni Timu nzuri.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic