September 27, 2019


SASA kazi imenoga kwenye michuano ya Sprite Bball Kings 2019 baada ya timu mbili kutinga fainali ya kuwania milioni kumi kwa mshindi wa kwanza kwa kushinda nusu fainali zao mbili walizocheza.
Timu ya Tamaduni ambayo iliibuka na ushindi wa vikapu 116 dhidi ya 65 vya KG Dallas kwenye mchezo wa nusu fainali ya pili huku Cornel Joseph akifunga pointi 28, rebounds 10 na assist 1. Katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali wikiendi iliyopita, Tamaduni iliibuka na ushindi wa vikapu 99 dhidi ya 78 vya KG Dallas.
 Mchenga Bball Stars iliibuka na ushindi wa vikapu 105 dhidi ya 72 vya Flying Dribblers huku mchezaji, Baraka Sadick wa Mchenga akifunga jumla ya pointi 49, rebounds 2 na assist 2. Katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali, Mchenga Bball Stars iliibuka na ushindi wa vikapu 95 dhidi ya 71 vya Flying Dribblers.
Fainali sasa itawakutanisha mabingwa watetezi Mchenga Bball Stars dhidi ya Tamaduni ambao walishinda kwenye nusu fainali mbili walizocheza na sasa ikiwa ni msimu wa tatu kwa michuano hii kufanyika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic