September 27, 2019

BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Issa Nampepeche anatarajia kupanda ulingoni dhidi ya Alli Hamis wa Morogoro katika pambano kuwapongeza mabondia walioshinda mikanda ya ubingwa kimataifa.
Katika pambano hilo linalofahamika  kama usiku wa mabingwa likiwa chini ya udhamini wa gazeti la Championi na +255 Global radio linatarajia kufanyika Oktoba 4, mwaka huu kwenye  Ukumbi wa Club 361 uliopo Mwenge, Dar.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Mratibu pambano  hilo, Selemani Semunyu alisema mipango imekamilika ikiwemo mabondia watakaocheza licha ya kupokea maombi mengi ya mabondia wanaotaka kushiriki kuonyesha furaha yao na kuwaunga mkono mabondia waliofanya vizuri kimataifa.
 Semenyu amewataja mabondia watakaopongezwa siku hiyo ni Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’, Tony Rashidi ,Bruno Vifua Viwili na  Nassib Ramadhani kufuatia kuiletea sifa nchi kimataifa.
"Serikali na Wabunge wamewapongeza lakini wadau na mashabiki sasa huu ndio wasaa wa kuwapongeza hata kama kuna zawadi ya kuwapa hii ndio sehemu moja lakini  tunawapongeza kwa pambano.
"Watakaofanya vizuri katika pambano hili wataweza kupata nafasi katika pambano la Desemba, mwaka huu katika pambano kubwa ambalo tumejipanga kulifanya.
Mapambano mengine siku hiyo yatakuwa ni Ibrahim Makubi  dhidi ya Abdallah Kingolwira, Maganga Kulwa  na Said Sudi, Hashimu Msungo vs Epson Lewis  wakati Salumu Omari atamalizana na  Ramadhani Chicho.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic