December 26, 2019


Chelsea wanapanga uhamisho wa mshambuliaji wa RB Leipzig na Ujerumani Timo Werner, 23. (Express)

Kiungo wa kati wa kati Mfaransa Paul Pogba, 26, anataka kundoka Manchester United na kujiunga tena na klabu yake ya zamani ya Juventus. (Calciomercato - in Italian)

Barcelona itajaribu kusaini tena mkataba na mshambuliaji wa Paris St-Germain na Brazil Neymar, 27, katika msimu wa uhamisho wa majira ya joto. (Goal)

Barcelona itajaribu kusaini tena mkataba na mshambuliaji wa Paris St-Germain na Brazil Neymar
Mshambuliaji wa Croatia Mario Mandzukic, 33, amemaliza tetesi juu ya hali yake ya baadae kwa kukamilisha taratibu za kuhamia klabu ya Al-Duhail ya Qatari licha ya kwamba Manchester United kumtaka. (Mail)

Manchester United wako tayari kumpa Mnorway Erling Haaland mwenye umri wa miaka 19 anayecheza katika safu ya mashambulizi mkataba wa pauni 200,000-kwa wiki kujiunga nao kutoka Red Bull Salzburg. (Sun)

Kiungo wa kati wa Leicester na England James Maddison, mwenye umri wa miaka 23, anatarajiwa kuwasiliana na Manchester United kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo kwa pauni milioni 80 msimu ujao wa majira ya joto. (Daily Star)

James Maddison, anatarajiwa kuwasiliana na Manchester United kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo.
Monaco wamejiunga na AC Milan na Manchester United katika harakati za kusaini mkataba na kiungo wa kati-nyuma wa Barcelona Mfaransa Jean-Clair Todibo, mwenye umri wa miaka 19. (Calciomercato)

Meneja anayekabiliwa na shinikizo wa West Ham Manuel Pellegrini anahitaji kusaini mikataba na wachezaji wanne mwezi Januari lakini wanaweza kumuacha mlinzi wao Issa Diop, 22, aondoke. (Express).

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic