SVEN Vanderbroek Kocha Mkuu wa Simba raia wa Ubelgiji na Seleman
Matola ambaye ni kocha msaidizi wana kibarua kizito ndani ya dakika 270 ambazo
ni sawa na mechi tatu kusaka pointi tisa za kufungia mwaka 2019.
Simba ambayo iliongozwa na Patrick Aussems aliyefukuzwa baada ya
kuongoza mechi 10 za ligi, ilishinda mechi 8 na kuambulia sare moja mbele ya
Tanzania Prisons na kupoteza mechi moja mbele ya Mwadui FC ipo nafasi ya kwanza
ikiwa na pointi 25 itaanza kuzimega dakika 270 za hatari Jumatano ya leo
Desemba 25.
Vanderbroek tayari ameonja utamu wa benchi la Simba kwa kupata
ushindi wa mabao 6-0 mchezo wake wa kwanza ambao ulikuwa ni wa kombe la
Shirikisho mbele ya Arusha FC leo atakaa benchi kwenye mchezo wa kwanza
utakaochezwa uwanja wa Uhuru.
Simba itamenyana na Lipuli ya Iringa Desemba 25 kisha Desemba 28
itamenyana na KMC kabla ya kufunga mwaka na Ndanda FC Desemba 31 kukamilisha
dakika 270 za hatari za kusaka pointi tatu zitakazochezwa uwanja wa Uhuru.
Akizungumza na Saleh Jembe, Seleman Matola amesema kuwa
wanatambua umuhimu wa mechi zao zote na zinaugumu wa kutosha jambo ambalo
linawafanya wazipigie hesabu kwa umakini na kuwataka mashabiki wajitokeze kwa
wingi kuipa sapoti timu yao.
0 COMMENTS:
Post a Comment