Inaelezwa kuwa klabu ya Simba imekamilisha Usajili wa beki wa timu ya Taifa ya Tanzania na Klabu ya Coastal Union ya Tanga Bakari Nondo Mwamnyeto.
Taarifa zinasema kuwa beki huyo atabaki Coastal Union kwa mkopo mpaka mwisho wa msimu huu na ujao atajiunga na Simba.
Awali watani zao wa jadi Yanga walikuwa wanawania saini ya mchezaji huyo lakini walishindwana dau baada ya kuwa kubwa.
Hela mnayo na Ingekuwa Hakuna msingesajili wachezaji kwa mamilioni halafu mkawafukuza baada ya mwezi mmoja
ReplyDeleteHii ni mbinu mbadala ya kumdhoofisha yanga ni kama tulivyofanya kwa niyonzima tulimsajiri lakini hatukumtumia, hata huyo wa ud songo ingawa tumemsajiri lakini tunaweza tusimtumie ili mradi yanga izidi kupata maumivu kwani kisasi cha mbui twite ni cha kudumu
ReplyDeleteHivi ni kweli hamkumtumia Niyonzima? Kwani alikuwa na mkataba wa miaka mingapi? Na je, alivunja mkataba au alimaliza mkataba was miaka yote 2? Hakika Yanga inawapa shida sana Simba na hiyo shida haitaisha. Punguzeni mapovu
ReplyDeleteYanga inawapa simba shida ktk jambo gani?
ReplyDelete