December 30, 2019


Mrembo wa Kirusi mwenye mvuto wa aina yake, Viktoria Odintcova, amedai kuwa aliikaushia na kuifutilia mbali meseji aliyotumiwa na supastaa Cristiano Ronaldo baada ya fowadi huyo wa Juventus, kumtumia ujumbe Instagram.

Mrembo huyo, 34, mwenye wafuasi milioni tano kwenye Instagram, amefunguka kuwa aliitosa meseji ya staa huyo miezi kadhaa iliyopita.

“Aliniandikia ujumbe mfupi. Ilikuwa ni zamani kidogo. Aliandika hivi, “Mambo, mzima wewe?”

“Nilifuta meseji hiyo na sikujibu,” alisema mrembo huyo.

Aliongeza: “Sikutaka kumpa nafasi, kwa sababu nawajua wanawake wengine aliowaandikia, kwa hiyo nilielewa lengo lake mapema.”

Ronaldo kwa sasa yupo penzini na mrembo Georgina Rodriguez tangu 2016 na wana mtoto mmoja wa kike pamoja aitwaye Alana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic