December 10, 2019


Uongozi wa klabu ya Yanga umesema utalitolea ufafanuzi wa kina suala la wachezaji wake wa kigeni kuondoka klabuni hapo.

Juzi zilienea taarifa za wachezaji Lamine Moro, David Molinga, Juma Balinya na Sadney Urikhob kutangaza kuachana na timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Twiga, Kariakoo.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu, Hassan Bumbuli, amesema watalitolea ufafanuzi wa kina leo na akiwataka wanayanga kutulia akisema kila kitu kitakuwa sawa.

Bumbuli ameeleza wataeleza kila kitu na mustakbali mzima wa wachezaji hao ambao wametekea vyombo vya habari katika medani za soka hivi sasa.


6 COMMENTS:

  1. Walipwe chao tatizo kumalizika wala haihitaji ufafanuzi wowote

    ReplyDelete
  2. Kwani tatizo ni ufafanuzi au madai yao siyo stahili?

    ReplyDelete
  3. walipeni UFAFANUZI mumalize shida zo

    ReplyDelete
  4. SASA TUMEJUA SABABU YA KUFUKUZWA ZAHERA , WALISHAJUA KUA SIKU HII ITAFIKA NA ZAHERA ATAPASUA UKWELI WOTE BILA CHENGA - SIJUI UBABAISHAJI UTAISHA LINI KATIKA VILABU VYETU .

    ReplyDelete
  5. Almuradi kila mmoja anachochea moto wake na huku kusajili dirisha dogo. Mambo hayaingii akilini hata kidogo Jee na Hao waliokubaliwa kuondoka kweli itakuwa salama Bila ya kudai chao

    ReplyDelete
  6. Mabadiliko ya Uendeshaji na kuifanya timu kuingia kwenye uwekezaji .....NINASHANGAA M/KITI ANASEMA ILE KAMATI ILIYOUNDWA INAENDELEA NA MCHAKATO KUTOKA MWAKA JUZI IMEKUWA NA VIKAO VINGI SANA YAANI WANASEMA MPAKA MWAKANI MWEZI WA 6....SASA WATAKUWA WAMECHUKUA MWAKA. 1 1/2...HUKU MNALIA GHARAMA ZA UENDESHAJI NA MAPATO HAYALINGANI NA MATUMIZI........MNATEGEMEA KUONGEZA WANACHAMA KUANDIKISHA WANACHAMA ILI MPATE FEES ILI ZIENDESHE KLABU KUBWA KAMA YANGA??? DAWA NI KUINGIA UBIA/UWEKEZAJI NDANI YA SIKU 60 HAKUNA MUDA WA KUSUBIRI KWAKUWA MMESHAPOTEZA MUDA MWINGI KATIKA MICHAKATO....KUNA VITU VINATAKIWA MITAJI MIKUBWA YA FEDHA KAMA USAJILI, KAMBI, POSHO, UJENZI WA VIWANJA VYA MAZOEZI (KIGAMBONI & KAUNDA) AMBAPO NI MATAJIRI WENYE UWEZO WA KIFEDHA WANAWEZA KUTATUA HILI.....MSIWE NA MAWAZO YA KARNE YA 18...KUTAFUTA MICHANGO KUTOKANA NA KUINGIZA WANACHAMA WAPYA HIZO NI NDOTO HAMUWEZI KUFANIKIWA...100% WANACHAMA KULIPA MICHANGO HAWAWEZI.....KUTOKANA NA UHALISIA WA UCHUMI UNAOBADILIKA KWA KASI

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic