January 3, 2020


Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara, amemtaka Kaimu Kocha wa Yanga, Boniface Mkwasa, kuhakikisha anacheza dhidi yao bila kufunguka.

Manara amemtaka Mkwasa kuhakikisha anacheza mchezo wa aina hiyo ili kuepukana na kichapo cha mbwa mwizi ambacho Yanga wanaweza kukipata.

Amemtaka acheze kwa kujilinda zaidi ili walau aweze kupunguza idadi ya mabao kama vile ambavyo Kocha wa Ndanda FC, Meja Mstaafu, Jenerali Abdul Mingange ambaye aliweza kufungwa mabao 2-0 dhidi ya Simba mechi ya mwisho.

"Kama Mkwasa anataka atoke salama katika mechi ya Jumamosi ni vema akacheza mchezo wa kufunguka.

"Hii itasaidia asiweze kufungwa mabao mengi, lakini akicheza bila kujilinda kwakweli ataondoka na aibu".













5 COMMENTS:

  1. Aibu gani hii kwa mwandishi!!!!Eti Meja mstaafu,Jenerali !!!!!! Shit hole blog

    ReplyDelete
  2. Mmeshanununua mechi. Mbona UD Songo walifunguka hamkuwafunga? Sawa endeleeni mtaona faida yake.

    ReplyDelete
  3. Mikia FC mnatapatapa tu,nyie ndio mnahofu kuliko Yanga wenyewe,mna timu gani ya kuwasumbua yanga? mbona mwadui fc walifunguka na mkala kichapo vilevile,na huyo kishingo wenu hiyo tar4 lazima mumtimue kazi

    ReplyDelete
  4. Acha kutoa povu hata mtoto mdogo ukimuuliza atakujibu alafu wewe unatuletea mbwembwe zako zisizoeleweka,Yanga mna taabu sana yani utadhani mnasajili wachezaji kutoka bacelona na man u kumbe mnasajili madude yasiyoeleweka bado kila kukicha mnapambwa magazetini kweli timu ya wananchi,na tayari mmeshaona mambo magumu mnaanza eti simba wamenunua mechi huo ni upumbavu uliokithiri acheni ujinga fanyeni mambo kama taasisi tena inayoongozwa na wasomi,huo ni njinga uliokithiri.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Simba nayo ni Taasisi au timu ya familia ya Mo! Yeye ndio anasema Aussems atoke Sven aingie. Wengine wote vi araka tu hamna kauli. Ukiambia utuambie chanzo cha mapato cha Simba sijui kama utaweza. Ukituambia kwa nini Aussems aliondoshwa ata amehojiwa hajui. Hiyo timu mnayoshangilia ni ya Mo! Nendeni mkafufue Simba yenu ya pale Msimbazi. Simba hii ni ya Masaki ndio mipango yote inafanyika. Viongozi waliobaki ni vibaraka. Viongozi wa kweli wa Simba walishaondoka siku nyingi.

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic