January 2, 2020

2 COMMENTS:

  1. Huyu jamaa ni professional hasa yaani unaona raha kumsikiliza tu akisema.Sina uweledi nae kwa maana yakwamba si mfahamu wasifu wake wa ndani ila wazungu wanamsemo usemao the first impression is the lasting impression when meeting someone for the first time.kwa maana yakwamba nyota njema huonekana mapema, kwa misemo yetu ya kiswahili.Nataka kusema tu kongole kwa Mo na wasaidizi wake pale Simba na tunawaombea mafanikio zaidi katika utendaji kwenye mwaka huu mpya. Moja ya vitu vinavyorejesha nyuma taasisi zetu kushindwa kupiga hatua ni kukosa watu sahihi wa kuziongoza. Na kiasi fulani nawaonea huruma sana Simba kwakuwa wamejitoa muhanga kwenda next level wakati taasisi zetu kuu zianazoisimamia Simba kwa maana ya TFF na serikali kwa ujumla sina hakika kama zipo tayari kwenda next level vile vile? Tunaona jitihada za Raisi wa TFF bwana Karia anajitajihidi kiasi chake kusema ukweli na moja ya sifa amabayo inamfanya awe tofauti na maraisi wengine waliopita wa TTF ni kule kuwa msikivu kusikiliza mawazo ya wadau wa soka nchini,kongole kwa hilo mwehashimiwa Karia.Ila hapa cha kujiuliza je bwana Karia ana watu au wasaidizi sahihi hasa wa kumsaidia kaliba ya bwana Masingisa? Mpira wa miguu ni serious business sio biashara ya mchezo mchezo lazima TFF na Nchi zijidhatiti hasa katika kuhakikisha tunakuwa kwenye level ya heshima kwenye mpira la sivyo jitihada za Simba na Azam na wengine wanaofuata zitaishia kusikojulikana. Simba na Azam hapana shaka ni msaada kwa nchi yetu na serikali katika kuinua kiwango cha mchezo wa mpira wa miguu nchini hapana ubishi juu ya hilo,katika kuleta ajira bora kwa vijana,katika kuitangaza nchi yetu,katika kuwaweka wananchi katika hali ya kujiliwaza kutoka katika mawazo ovu kama vile misiba na uchungu wa maisha. Na hapana shaka michezo ni furaha na furaha inakuwa furaha zaidi kama timu zetu zitaku zinafanya vizuri kwa hivyo hapana shaka kwa mawazo yangu nguvu za serikali katika kuzisapoti klabu zetu kuhakikisha zinafikia malengo ya kimaendeleo ni lazima na sio hiyari. Mfano, usiingie ndani,angalia kwa pembeni tu basi utaona pale simba kumeekezwa sio mchezo. Kuanzia wafanyakazi,miundo mbinu nakadhalika. Ukianzia kwa wachezaji wa kigeni,wataalam wa mazoezi kwa wachezaji yaani madaktari na makocha utaona Simba ina wataalam wa kigeni karibia ishirini ni mradi wa gharama ila hata reli tulikuwa nao siku nyingi lakini katika kuhakikisha tunakwenda kunako next level katika huduma za reli nchini ndio sasa tunaowataalam wa kutujengea reli mpya ya standard gauge ni kama tunaanza upya na mikakati imara zaidi tunasema nyumba imara ni msingi imara. .Na nnaimani tunahitaji mikakaakti ya standard gauge kwenye Riadha na Ngumi vile vile hizi taasisi zinahitaji kufumuliwa na kusukwa tena upya. Ikiwezekana wafukuzwe watu wote wanaosimamia hizo taasisi na kuleta watendaji wapya hata wataalam wa kigeni wenye vigezo kuziendesha.
    Watanzania tunaweza ila la kuzingatia ni uzalendo kwanza na tuwache kufanya kazi kitapeli kwani hakuna njia ya mkato katika kufikia malengo.Tunaweza tu kuwa wabunifu wa kurahisha njia za kufikia malengo kwa haraka, ila ukweli na uaminifu wetu katika kazi ndio utakao tutowa watanzania na sio ujanja ujanja na ndio maana nasema bila ya aibu kuwa zidumu fikra za Magufuli milele kwenye Taifa hili la Tanzania ama the Garden nation of all beautiful gardens in Africa. Mungu ibariki Tanzania,Amen.
    Kheri za mwaka mpya na maoni sio matusi Ahsante.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mfumo wa Uendeshaji wa Klabu ya Simba ni wa kisasa zaidi na unafaa kuigwa....kuiendesha klabu kubwa kama Yanga kwa staili ya ufadhili ni karne ya 19....ukiwa unaendesha kwa mfumo wa hisa na uwekezaji klabu inakuwa kampuni inaajiri watu wa kufanya kazi kuiendesha kama kampuni na mipango yake inakuwa ya kisasa (wataalamu wa soka/walimu waliobobea, wataalamu wa fitness, Lishe ya wachezaji, Wachua misuli, afya za wachezaji, match analysts, kambi bora na ratiba bora ya mazoezi, viwanja vya kisasa vya mazoezi na academy za soka kwa vijana) ..sio mwanachama huyu anateuliwa kwenye kamati hii au Ile, wachezaji mishahara inachelewa baadaye wanagoma, matibabu ya wachezaji kuchukua mwaka, ni baadhi ya changamoto za kuiendesha klabu kizamani kama Yanga

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic