January 29, 2020


Kocha Mkuu wa Klabu ya Yanga, Luc Eymael amesema hapendi kuona mchezaji wake, kiungo Bernard Morrison akiwadhalilisha wapinzani wake kwa staili yake ya uchezaji.

Kauli hiyo ameitoa Januari 26, 2020 baada ya kumalizika kwa mchezo wake na Timu ya Tanzania Prisons katika Kombe la Shirikisho, ‘Azam Sports Federation Cup (ASFC)’ ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa 2-0.

Kocha Eymael amesema kuwa ameshaoongea na mchezaji huyo juu ya aina yake ya mchezo ambao unawadhalilisha wapinzani.

“Mimi sipendezwi kuona mtu anawadhalilisha wengine, ukifanya vile Ulaya utafanyiwa ‘tackle’ ya hatari sana. Ukiangalia Liverpool, Mo Salah anaweza kufanya hivi?, Sadio Mane anafanya hivi? hapana na mimi nimeshaongea na Morrison nimemwambia sipendi staili hii”, amesema Eymael na kuongeza kuwa;

“Mashabiki wanapenda kuona mchezaji akifanya hivyo lakini kwangu mimi ni kutowaheshimu wapinzani na nimeshamwambia Bernard Morrison.”

Katika michezo miwili ya Yanga, Morrison ametokea kupendwa na mashabiki wa klabu hiyo kutokana na aina ya uchezaji wake uliojaa mbwembwe za kupanda juu ya mpira huku mashabiki wa timu hiyo wakimpa sifa lukuki na kudai Morrison ni wakina Chama 500 (Chama ni mchezaji wa Simba).

2 COMMENTS:

  1. YANGA malimbukeni kwani kocha wao wenyewe keshashtuka kuwa jamaa ni mchezaji wa hovyo. Kuna mchezaji mwenye adabu ndani ya uwanja kama Chama mwamba wa Lusaka? Hivyo chama alishapata angalau kuonywa na mwamuzi kwa vitendo vya kijinga uwanjani tangu atuwe bongo.

    ReplyDelete
  2. Mtua naona inaonekana Hana maarifa ya anacho ongea, mbona alichofanya Marrison sio kitu kigeni duniani.
    Punguza povu: angalia link below:
    https://youtu.be/_wjcUgvzq6g

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic