January 12, 2020




Yanga imeajiri kocha mwingine ajulikanaye kwa jina la Riedoh Berdien, raia wa Afrika Kusini.


Berdien atakuwa msaidizi wa Luc Eymael na kazi yake kubwa ni fiziki ya miili ya wachezaji. Na taarifa zimeeleza atakaa kwa muda kuhakikisha kikosi kinakuwa na fiziki ya kutosha.


Kabla ya kukubaliana na Yanga, Berdien amewahi kufanya kazi sehemu mbalimbali ikiwemo nchini Afrika Kusini katika klabu za Chippa United na Free State.


Pamoja na hivyo, Berdien amekuwa chini ya makocha wawili tofauti waliowahi kuifundisha Yanga.



Aliwahi kufanya kazi na Kocha Mserbia, Sredejovic Milutin maarufu kama Micho lakini akafanya kazi na kocha mwingine wa zamani wa Yanga, Tom Saintfiet katika klabu hiyo ya Free State ya Afrika Kusini lakini baadaye timu ya taifa ya Togo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic