February 23, 2020



BAKARI Mwamnyeto, nahodha wa Coastal Union amesema wamejipanga kulipa kisasi kwa Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa leo Uwanja wa Mkwakwani.

Kwenye mchezo wa kwanza uliozikutanisha timu hizo Uwanja wa Uhuru jijini Dar, Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Abdulaziz Makame.

Coastal Union inaingia katika mchezo huo ikiwa na maumivu ya kufungwa mabao 2-1 na Ruvu Shooting,Yanga ikitoka kuambulia sare ya 1-1 dhidi ya Polisi Tanzania.

“Tunafahamu mchezo utakuwa mgumu ndani ya dakika zote tisini kutokana na presha ya mashabiki wa pande zote mbili, lakini tumejipanga kulipa kisasi, hatutaki kuona tunafungwa tena na Yanga,” amesema beki huyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic