NAMUNGO FC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Azam FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa leo Februari 22 Uwanja wa Majaliwa.
Bao pekee la ushindi lilipachikwa kimiani na mshambuliaji mzawa namba moja ndani ya Namungo, Reliants Lusajo dakika ya 60 na kuwafanya Azam FC kushindwa kupindua meza kibabe.
Kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Chamazi, Azam FC ilishinda kwa mabao 2-1 hivyo leo Namungo imelipa kisasi.
Ikiwa ugenini Azam FC imepukutisha pointi tano kati ya sita iliyokuwa inazisaka kwa kuambulia pointi moja mbele ya Ndanda FC kwenye sare ya kufungana bao 1-1.







0 COMMENTS:
Post a Comment