KOCHA Mkuu wa
Kitayosce FC ya Tabora, Boniface Kiwale, amesema wamejipanga kucheza kufa au
kupona dhidi ya Ndanda katika mchezo wa Kombe la FA utakaochezwa Februari 26,
mwaka huu kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.
Akizungumza
na Championi Jumamosi, Kiwale amesema: "Nimekuwa nikiwafuatilia Ndanda kwa
muda mrefu sana na sisi kama Kitayosce tumejiandaa kuhakikisha kwamba tunapata
matokeo mazuri japokuwa mchezo huo utakuwa mgumu.
"Nimeona
kwa mwezi huu Ndanda wamekuwa wakifanya vizuri kwenye ligi kuu hasa kwa michezo
yao mitano iliyopita, lakini hilo halituogopeshi zaidi ya kwamba tunajipanga
kupambana kufa au kupona ili tuweze kushinda."








0 COMMENTS:
Post a Comment