March 5, 2020

AGREY Moriss, nahodha wa Azam FC amesema kuwa walishindwa kupata ushindi mbele ya Simba jana Uwanja wa Taifa kutokana na makosa yao wenyewe.

Kwenye mchezo uliochezwa Machi 4, Azam ilikubali kichapo cha mabao 3-2 kutoka kwa Simba na kupeperusha pointi tatu muhimu.

"Tulianza kwa kasi na kushindwa kuzitumia nafasi ambazo tulizipata wapinzani wetu waliweza kutumia nafasi walizotengeneza wakatushinda na huu ndio mpira na haya ni matokoe, tunajipanga," amesema. 

Azam FC imepigwa nje ndani na Simba msimu kwa jumla ya mabao 4-2, mchezo wa kwanza walifungwa bao 1-0 na mchezo wa pili walifungwa mabao 3-2.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic