March 12, 2020


SERGIO Ramos, nahodha wa timu ya Real Madrid amesema kuwa wana kazi ngumu ya kufanya ili kufikia malengo waliyojiwekea ya kutwaa ubingwa wa La Liga .

Real Madrid ilikubali kichapo cha mabao 2-1 mbele ya Betis jambo lililowaumiza wachezaji wengi ndani ya kikosi hicho.

Ramos amesema kuwa bado nafasi ya kutwaa ubingwa ipo lakini haitatimia iwapo watashindwa kujikosoa pale walipokosea ili wawe bora zaidi. 


"Tunapaswa tujikosoe wenyewe na kuona namna gani tutakuwa bora, ili tutwae ubingwa ni lazima kuboresha utendaji wetu wa kazi na kutimiza majukumu yetu kwa bidii," amesema.

Madrid ipo nafasi ya pili na ina pointi 56 imecheza mechi 27 sawa na Barcelona ambao ni vinara wana pointi 58.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic