Akizungumza na Saleh Jembe, Thiery amesema kuwa anajivunia uwezo wa wachezaji wake kupambana ndani ya uwanja jambo linalompa matumaini ya kupata matokeo mbele ya Mtibwa Sugar.
“Tupo vizuri na wachezaji wangu wamekuwa wakionyesha uwezo ambao unanishangaza licha ya kupitia kwenye ugumu wa ratiba hasa kusafiri kunatufanya tucheze chini ya uwezo wetu ambao tunao ila tutapambana bila kuchoka,” amesema Thiery.
Namungo FC ipo nafasi ya nne ikiwa imecheza mechi 24 imejikusanyia pointi 46.
0 COMMENTS:
Post a Comment