June 21, 2020

KUPOTEZA kwa kufungwa mabao 2-0 jana Juni 20 mbele ya JKT Tanzania kunazidi kuizamisha kwenye ugumu wa kujitoa kwenye mstari wa kushuka daraja Klabu ya Singida United.

Jana Uwanja wa Jamhuri, Singida United ilishindwa kufurukuta mbele ya JKT Tanzania na kukubali pointi tatu kuyeyuka jumla.

Mabao ya JKT Tanzania yalipachikwa kimiani na Musa Said dakika ya 11 na Hafidh Mussa dakika ya 61.

Singida United ipo nafasi ya 20 ikiwa na pointi 15 baada ya kucheza mechi 30, imebakiwa na mechi nane ili kukamilisha mzunguko wa pili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic