UWANJA wa Samora, majira ya saa 10:00 jioni leo kunatarajiwa kuwa
na mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya Lipuli na Yanga huku rekodi zikiwabeba wana
Jangwani.
Lipuli iliyo chini ya Nzeyimana Mailo tangu ilipopanda daraja
msimu wa 2017/18 imekutana mara tano kwenye mechi za ligi,Yanga imeshinda
mechi tatu na Lipuli imeambulia ushindi mara moja na kuambilia sare moja.
Yanga imefunga jumla ya mabao sita huku Lipuli ikifunga jumla ya
mabao matatu na kufanya jumla mabao kuwa tisa.
Matokeo yao yalikuwa namna hii: 2017/18, Lipuli 0-2 Yanga, Yanga
1-1 Lipuli msimu wa 2019/20, Lipuli 1-0 Yanga, Yanga 1-0 Lipuli na msimu wa
2019/20, Yanga 2-1 Lipuli.
Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ambapo Lipuli inahaha kusaka tiketi ya kubaki ndani ya ligi huku Yanga ikipambania nafasi ya pili.
Lipuli ipo nafasi ya 13 ikiwa na pointi 44 huku Yanga ikiwa nafasi ya tatu na pointi 69 sawa na Azam FC ambayo ipo nafasi ya pili.
0 COMMENTS:
Post a Comment