UONGOZI wa Yanga umeeleza kuwa umeachana rasmi na nyota wake saba kwenye kikao ambacho kmefanyika leo.
Wachezaji hao ni wale ambao mikataba yao ndani ya Klabu hiyo yenye maskani yake pale Janganwani imefika tamati na hawajaongeza dili jingine.
Hii hapa orodha ya wachezaji ambao wameachwa na Yanga hivyo hawatakuwa ndani ya kikosi kwa msimu wa 2020/21:-Papy Tshishimbi nahodha wa Yanga, David Molinga mshambulaiji namba moja ambaye ametupia mabao 11 ndani ya kikosi na pasi moja ya baoa.
Mrisho Ngassa winga aliyekuwa amewaka mwishoni mwa msimu na mchezo wake wa mwisho alihusika kutoa pasi kwa Molinga. Jaffary Mohamed kiraka rasta kichwani ,Tariq Seif.
Andrew Vincent beki mwenye manywele mwengi kichwani na Mohamed Issa maarufu kama Mo Banka.
Duh!
ReplyDeleteWawalipe
ReplyDeleteHaya ndiyo matatizo ya kusoma kichwa cha habari na ku-comment. Unapenda kuchangia, lkn mvivu kusoma habari, matokeo yake unachangia lolote linalokuja kichwani. Falsafa ya hapa kazi tu inahusu hata katika hili
DeleteKwa Jafary yanga wamebugi. Lakini ngoja Tuwaachie wataalam wa soka wengine sisi ni mashabiki
ReplyDeleteNi mchango wenye madini kichwani. Kwani sisi ni mashabiki, wataalam walioshauri wanajua kiufundi timu ilikwama wapi hadi isifanye vizuri
Delete